• Matukio ndani ya UDA yanaonyesha upungufu wa sera.
    Aug 1 2024
    Matukio yanayoendelea ndani ya chama cha UDA ni dhihirisho tosha la umbali wa safari yetu kuwa na vyama vya kisiasa vyenye sera na msimamo. Vyetu ni vyama vinavyotumiwa tu kuwa daraja la kuingia mamlakani na baada ya uchaguzi, kudondoshwa kama kaa moto.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.
  • Bunge la Kitaifa Laanza Msasa wa Mawaziri Walioteuliwa
    Jul 31 2024
    Bunge la Kitaifa linaanza kuwapiga msasa Mawaziri walioteuliwa na Rais William Ruto, katika Baraza jipya alilotangaza. Hii ni fursa adimu kwa Bunge kutekeleza wajibu wake wa Kikatiba na kuonesha kuwa ni taasisi huru na inayojisimamia bila kushurutishwa na Serikali tendaji. Hii ni fursa ya Bunge kusafisha jina lake ambalo limekuwa si lolote la kujivunia.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.
  • Kumbukumbu ya Hatua za Kinidhamu na Maswali ya Hatima
    Jul 30 2024
    Chama cha ODM kimeendelea kutoa msimamo kinzani kuhusu hatua ya viongozi wake wakuu kujumuishwa serikalini, na kuibua kumbukumbu ya hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya Wabunge wake waliotangaza msimamo wao wa kushirikiana na serikali baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita. Je, viongozi hawa wakuu wa chama hiki watachukuliwa hatua zozote. Kama sivyo, basi tusihadaiwe zaidi.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    4 Min.
  • Heshimu Wanahabari na Taaluma ya Uanahabari
    Jul 25 2024
    Maandamano yaliyofanywa na wanahabari nchini hayashinikizi lolote nje ya Katiba ya nchi. Yanashinikiza tu taaluma ya uanahabari kuheshimiwa na haki za wanahabari kulindwa kama ilivyo katika sheria za nchi. Wanahabari sio wahalifu, wao ni mwito wa kuitumikia nchi na wananchi wake.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.
  • Rais Ruto Askilize Vijana Kwa Matendo, Sio Vitisho: Sepetuko
    Jul 24 2024
    Maandamano yanayoendelea dhidi ya serikali yanamaanisha kuwa Rais William Ruto atastahili kuwasikiliza zaidi vijana wanaoandamana. Kusikiliza huku hakuwezekani katika mazingiraya kujipiga kifua na vitisho. Kusikiliza huku ni zaidi kupitia kwa matendo.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.
  • Bustani ya Demokrasia
    Jul 22 2024
    Harakati ambayo imekuwa ikiendelezwa dhidi ya serikali lazima ikuze taifa linalosikiliza. Linalosikiliza kwa lengo la kuelewa, na kukumbuka kuwa serikali ni raia na sio vinginevyo. Government by the people, for the people...
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.
  • Kamwe tusiruhusu wahuni kurejea katika mitaa yetu, na siasa zetu.
    Jul 19 2024
    Maandamano dhidi ya serikali yameingiliwa na wahuni ambao nia yao ni kupora, kujeruhi na hata kuua na kuharibu. Jumatano wiki hii, wahuni pia wametatiza mkutano wa Azimio, wakisababisha purukushani na majeraha kwa wanahabari. Ni wakati wahuni hawa na wafadhili wao wakabiliwe vilivyo.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    4 Min.
  • Kuendeleza Uhuru wa Vyombo vya Habari ni Kudumisha Demokrasia ya Kenya
    Jul 18 2024
    Kukamatwa kwa mwanahabari mtajika Macharia Gaitho katika mazingira ya kudhalilisha na kuhujumu haki za mtu, siku moja tu baada ya mwanahabari wa Kameme kufyatuliwa risasi na polisi huko Nakuru alipokuwa akiangazia maandamano dhidi ya serikali kunaonesha kuchipuka tena kwa majaribio ya kudunisha uhuru wa vyombo vya habari unaolindwa Kikatiba. Kamwe tusikubali hilo kufanyika, uhuru wa wanahabari na vyombo vya habari ni mhimili muhimu mno wa demokrasia ya Kenya.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    5 Min.