Folgen

  • Mbona Magari ya Umeme? | Uchumi na Biashara Podcast
    Dec 11 2022
    Baadhi ya kampuni za uagizaji na uuzaji wa magari nchini zimebadili mwelekeo na sasa zinajitosa katika uagizaji wa magari yanayotumia umeme. Kampuni ya hivi punde kufanya hivyo ni ya BasiGo na ya kwanza kuagiza mabasi 15 ya umeme ambayo yalitengenezwa na Kampuni ya BYD Automotive iliyo nchini Uchina. Mabasi haya tayari yamewasili nchini kupitia Bandari ya Mombasa na yanatarajiwa kutoa huduma za uchukuzi jijini Nairobi. Lakini je, mbona wafanyabiashara waanze kufuata muelekeo wa uagizaji wa magari ya umeme? Robert Menza amewahoji baadhi ya washikadau katika sekta hiyo
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    15 Min.
  • Kuvuma kwa Utalii Krisimasi na Mwaka Mpya | Uchumi na Biashara Podcast
    Nov 25 2022
    Huku msimu wa Krimasi na Mwaka Mpya ukikaribia Sekta ya Utalii inategemea sana msimu huu kuimarika kutokana na watalii wa mataifa ya kigeni wanaolenga kuzuru maeneo mbalimbali ya kitalii nchini. Mojawapo ya maeneo hayo ni eneo la Pwani hususani Kaunti ya Mombasa. Je, wafanyabiashara hasa wa hoteli za kitalii wamejiandaa vipi msimu huu? Robert Menza amezungumza na Josephat Iha ambaye ni Meneja wa Mauzo katika Mkahawa wa Massai Beach.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    22 Min.
  • Serikali saidia, biashara zetu zazorota | Uchumi na Biashara Podcast
    Oct 29 2022
    Licha ya serkali kuahidi kushughulikia changamoto za wafanyabiashara wadogo wadogo, bado mahangaiko yanashuhudiwa mwezi mmoja baada ya Kenya Kwanza kuchukua hatamu za uongozi. Wengi wa wafanyabiashara hao wanalalamikia kuongezwa kwa bei ya mafuta, na kusababisha hasara katika sekta ya matatu. Charles Macharia, mhudumu wa teksi na Jimmy Mwangi, mhudumu wa matatu wanatishia kugura biashara hii. Mwanahabari wetu Edwin Mbugua amefanya mazungumzo na baadhi ya wafanyabiashara hao katika Kaunti ya Nyeri.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    15 Min.
  • Nyumba za Bei Nafuu | Uchumi na Biashara Podcast
    Oct 25 2022
    Washikadau mbalimbali wanaunga mkono mpango wa ujenzi wa nyumba kwa bei nafuu unaoendelezwa na serikali, mfano mradi wa Buxton Point katika Kaunti ya Mombasa unaoendelezwa na mfanyabiashara, Suleiman Shahbal na Serikali ya Kaunti ya Mombasa. Robert Menza amezungumza na Martin Kariuki, anayesimamia uuzaji wa nyumba hizo.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    18 Min.
  • Uzalishaji wa mayai | Uchumi na Biashara Podcast
    Oct 24 2022
    Licha ya Shirika la Afya Dunia, WHO kushauri kuwa binadamu anafaa kula mayai 180 kwa mwaka, imebainika kwamba taifa la Kenya halijaafikia kiasi hicho takwimu zikionesha kuwa mayai 36 tu huliwa kwa wastani kulinganishwa na mataifa mengine mfano taifa jirani la Uganda na Afrika Mashariki. Hali hii imesababishwa na Wakenya kuzalisha mayai kwa wingi kwa minajili ya kufanya biashara ikilinganishwa na Uganda ambapo huzalishwa vijijini. Mwanahabari wetu Martin Ndiema amesema na wafanyabiashara wa mayai kubaini jinsi uzalishaji na ulaji huathiri biashara yao.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    10 Min.
  • GMO na hofu kuhusu bei masokoni | Uchumi na Biashara Podcast
    Oct 11 2022
    Katika Makala Uchumi na Biashara Podcast, mwanahabari wetu wa Kaunti ya Trans Nzoia, Martin Ndiema amesema na wakulima ili kubaini ikiwa wameridhia kupanda mimea iliyoboreshwa kwa njia ya kijenetiki yaani GMO. Wapo ambao wamekumbatia na wengine kuirai serikali kuutafakari upya kuhusu uamuzi huo wa Baraza la Mawaziri wa kupitisha GMO. Aidha, amesema na mtaalamu wa mimea akizamia ubora wa mazao ya mimea ya GMO, soko la kimataifa na usalama wa chakula kwa matumizi ya binadamu.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    9 Min.
  • Sarafu ya pamoja na boda huru Barani Afrika
    Sep 20 2022
    Leo kwenye Makala Uchumi na Biashara mwanahabari wetu wa Kaunti ya Trans Nzoia, Martin Ndiema anaangazia juhudi zinazowekwa na viongozi wa matabaka mbalimbali Barani Afrika kufanikisha kuwapo kwa sarafu moja inayopendekezwa kuitwa AFRO. Aidha amezamia suala la kuafikia boda huru kustawisha uchumi wa bara hili.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    8 Min.
  • Uchumi na Biashara Podcast; Kenya haina deni la shilingi trilioni 8.47, asema Jimmy Wanjigi
    Jul 29 2022
    Mfanyabiashara Jimmy Wanjigi sasa anapinga kwamba taifa lina deni la shilingi trilioni 8.47 jinsi ilivyochapishwa na Benki Kuu-CBK. Kulingana na Wanjigi, deni ni chini ya trilioni 3. Pia amedai fedha za mikopo ya ndani kwa ndani-domestic debts hazikutumika katika miradi ya serikali badala yake kuibwa.
    Mehr anzeigen Weniger anzeigen
    7 Min.